Kutoka “Police Fire Brigade” Hadi
“Jeshi la
Zimamoto Tanzania”
·
Sheria namba 14
ya mwaka 2007, chachu ya ufanisi wake
·
Lanufaika na
ushirikiano na JWTZ
Na Sgt.Hassan J.Mtengevu
Huduma
za Zimamoto Tanzania Bara zilianza wakati wa utawala wa kikoloni mara baada ya
vita kuu ya pili ya dunia mwaka 1945, ambapo kipindi hicho kulikuwa na kikosi
kimoja tu kilichoitwa Police Fire
Brigade kilichosimamiwa na Jeshi la Polisi.
Mwaka
1950 huduma hii iligawanywa katika makundi mawili ambayo ni Zimamoto ya
Manispaa iliyokuwa chini ya usimamizi wa Manispaa, na Zimamoto Viwanja vya
Ndege iliyokuwa chini ya usimamizi wa Idara ya Kazi.
Kutokana
na kupanuka kwa miji, viwanja vya ndege na bandari, vikosi vingine vya Zimamoto
vilianzishwa na kimojawapo ni Zimamoto Bandari chini ya usimamizi wa Mamlaka ya
Bandari.
Mwaka
1982 huduma ya Zimamoto viwanja vya ndege iliwekwa chini ya Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, wakati vikosi vya Zimamoto vya Manispaa na Miji viliwekwa chini
ya Ofisi ya Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais, vikisimamiwa na Wizara ya
Serikali za Tawala za mikoa na Miji.
Kutokana
na majukumu ya Zimamoto kusimamiwa na mamlaka tofauti, ufanisi wake haukuwa wa
kuridhisha, hivyo kuilazimu serikali kuangalia namna ya kuboresha huduma hiyo.
Mwaka
1985, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilipitisha sheria Na. 3
iliyoanzisha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ili kuifanya huduma hiyo itolewe
katika nidhamu ya kijeshi chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Katika
kuendelea kuboresha huduma za Zimamoto na Uokoaji, mwaka 2007 Bunge la Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania lilipitisha Sheria Na. 14 ya Zimamoto na Uokoaji yani
(Fire and Rescue Force Act) iliyoviweka vikosi vya Zimamoto na Uokoaji chini ya
kamandi moja.
Sheria
hii kwa kiasi kikubwa ilitoa fursa kwa Jeshi la Zimamoto na uokoaji kujipanga
upya kimuundo na kuweka mgawanyo wa majukumu wenye tija, ili kurahisisha utoaji
huduma ya zimamoto na uokoaji.
Sasa
hivi jeshi la Zimamoto na Uokoaji linaongozwa na Kamishna Jenerali anayesaidiwa
na Naibu Kamishna Jenerali, akifuatiwa na Makamishna watatu wanaoongoza divisheni
tatu za jeshi hilo ambazo ni utawala na fedha, oparasheni na tawi la usalama wa
umma na mali.
Chini
ya divisheni hizi kuna vitengo vinavyoongozwa na Makamishna Wasaidizi, ili
kutengeneza mfumo wa kiutendaji wenye kuleta tija katika utoaji huduma kwa
jamii.
Divisheni
ya Usalama wa Umma linahusika na kuzuia na kukabiliana na majanga kama moto,
matetemeko ya ardhi, mafuriko, na majanga mengine pindi yanapo tokea pamoja na
kufanya uchunguzi wa majanga hayo kubaini chanzo chake na kupanga mikakati ya
kukabiliananayo.
Kupitia
vitengo vilivyo chini yake, pia divisheni hii linahusika na kuelimisha jamii
juu ya majanga ya moto na uokaoji, kukagua majengo, kuandaa na kutekeleza
mipango ya kuzuia moto, kupanga na kukagua usalama wa ujenzi katika viwanda,
vituo vya mafuta na kemikali pamoja na vituo vinavyozalisha gesi.
Kwa
upande wa divisheni ya oparesheni, miongoni mwa majukumu yake ni kusimamia
mafunzo, kukagua huduma za zimamoto na uokoaji kwenye kanda pamoja na kufanya
tahmini ya madhara yaliyotokea kwenye majanga mbalimbali.
Majukumu
ya divisheni ya Utawala, rasilimali watu na fedha ni kufanya utafiti na mafunzo,
kusimamia uajiri, kuandaa na kutunza kumbukumbu za watumishi pamoja na maandalizi
na mapitio ya sheria ya moto na uokoaji na kanuni zake.
Pamoja
na muundo huo, Jeshi la Zimamoto pia limeweza kuboresha chuo chake ambacho
majukumu yake ni kuendeleza na kufanya mapitio ya muundo wa Zimamoto na
Uokoaji, kufanya utafiti kuhusu madhara ya matukio ya majanga ikiwa ni pamoja
na kulinganisha matokeo ya ndani na nje ya tafiti hizo.
Chuo
hiki pia kinatoa mafunzo yote kwa askari wa Jeshi hilo pamoja na mafunzo ya
nidhamu kwa maafisa, sambamba na mafunzo kwa wadau majanga mbalimbali wote pamoja
na wananchi kwa ujumla.
Pamoja
na changamoto kadhaa zinazolikabili Jeshi la Zimamoto, Jeshi hilo kwa kiasi
kikubwa limejitahidi kusambaza huduma zake kwa wananchi, kwa kweka vituo vya
zimamoto katika baadhi ya makao makuu ya mikoa, wilaya na maeneo mengine muhimu
nchi nzima.
Mafanikio
mengine ni Jeshi hilo kuwa na ushirikiano mkubwa na vyombo vingine vya ulinzi
na usalama, hivyo kuongeza wigo wa kiutendaji. Miongoni mwa matunda ya
ushirikiano huo ni pamoja na Jeshi la Magereza kukubali kutoa mafunzo ya
kijeshi ya awali, uongozi mdogo wa kati na uongozi wa juu ili kuwajengea uwezo
wa kiutendaji maafisa na askari wa Zimamoto.
Kwa
upande wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania, limekuwa karibu sana na
Jeshi la Zimamoto na Uokoaji katika maokozi pindi yanapotokea majanga makubwa
yanayotishia usalama wa watu na mali zao.
Kwa
mfano tarehe 03 Desemba 1989 Jeshi la Wananchi lilishirikiana na Zimamoto na
Uokoaji kukabiliana na moto uliotokea katika kampuni ya kusafisha mafuta ya
Tazama Tank Farm Dar es Salaam na kufanikiwa kuuzima.
Mwaka
2001 vyombo hivyo vilishirikiana tena kupambana na moto wa mafuta uliotokea
katika kinu cha kufua umeme yaani cha TANESCO eneo la Ubungo Dar es salaam na kufanikiwa kuuzima na
kuokoa maisha na mali za wakazi wa Jiji la Dar es Salaam.
Maeneo
mengine ni pamoja na ajali za MV SPICE ISLAND NA MV SCAGIT zilizotokea Zanzibar.
Ushirikiano
huu umeenda mbali zaidi ambapo ili kuzidi kusambaza huduma za zimamoto kwa
wananchi, JWTZ limeridhia kuruhusu ujenzi wa vituo vya Jeshi la Zimamoto kwenye
baadhi ya maeneo ya kambi zake za Lugalo, Mabibo, Kigamboni, Mbagala na
Gongolamboto.
Hii
inatokana na Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange kwa kushirikiana na
watendaji wa Jeshi hilo, kuwathamini watanzania na mchango wa Jeshi la Zimamoto
kwa jamii.
Kwa
hakika pamoja na kwamba historia ya Zimamoto inaonesha Jeshi hilo lilianza kwa
kusuausua, kwa jitihada za Serikali katika kurekebisha sheria na mazingira ya
utendaji wa Jeshi hilo na kwa ubunifu wa watendaji wa Jeshi hilo katika
kuliboresha, leo hii watanzania wameanza kunufaika na huduma yake.
Kilichopo
sasa ni kwa kila mmoja kwa nafasi yake kuhakikisha changamoto zinazolikabili
jeshi hilo zinapatiwa ufumbuzi, ili kuliboresha Jeshi hili kwa rasilimaliwatu
na vifaa hatimaye Taifa liwe na uwezo wa kukabiliana na majanga yanayohatarisha
usalama wa watu na mali zao.
Imeletwa
kwenu kwa hisani na usaidizi wa Cpl Ibrahim Luena.
©Public Relation
Education and Information-Fire and Rescue Singida
Hakika tunafurahia huduma za jeshi la zimamoto, japo kuna changa moto ndogondogo za kiutendaji hasa kwa askari wa jeshi hilo;
ReplyDelete1. askari kujihusha kutoa huduma zinazotolewa na na madelear ambao wapo kisheria na wanalipia vibali halali vinavyotolewa na jeshi ( certificate of competence)
na wanasahau majukumu yao ya msingi kabisa.